b Kum 11:14; 28:12; Za 65:9; 67:6; 68:9; 104:13; 147:8; Yer 5:24; Hos 6:3; Yoe 2:23; Zek 10:1; Ay 5:10; 14:9; Kut 23:24; Law 25:19
Leviticus 26:3-8
3 a“ ‘Ikiwa mtafuata amri zangu na kuwa waangalifu kutii maagizo yangu, 4 bnitawanyeshea mvua katika majira yake, nayo ardhi itatoa mazao yake, na miti ya mashambani itazaa matunda yake. 5 cKupura nafaka kwenu kutaendelea mpaka wakati wa kuvuna zabibu. Pia kuvuna zabibu kutaendelea mpaka wakati wa kupanda mbegu, nanyi mtakula na kushiba, na mtaishi salama katika nchi yenu. 6 d“ ‘Nitawapa amani katika nchi, mpate kulala pasipo kutiwa hofu na yeyote. Nitawaondoa wanyama wakali watoke kwenye nchi, nao upanga hautapita katika nchi yenu. 7 eMtawafukuza adui zenu, nanyi mtawaua kwa upanga mbele yenu. 8 fWatu wenu watano watafukuza adui mia, watu wenu mia watafukuza adui elfu kumi, nao adui zenu wataanguka kwa upanga mbele yenu.
Copyright information for
SwhKC